Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 8:26-33 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza.” (Njia hiyo hupita jangwani).

27. Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa mkurugenzi maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.

28. Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.

29. Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”

30. Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”

31. Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kuniongoza?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.

32. Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii:“Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa;kimya kama vile mwanakondoo anapokatwa manyoya,yeye hakutoa sauti hata kidogo.

33. Alifedheheshwa na kunyimwa haki.Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake,kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”

Kusoma sura kamili Matendo 8