Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 2:17-30 Biblia Habari Njema (BHN)

17. ‘Katika siku zile za mwisho, asema Bwana,nitawamiminia binadamu wote Roho wangu.Watoto wenu wa kiume na wa kike watatoa unabii,vijana wenu wataona maono,na wazee wenu wataota ndoto.

18. Naam, hata watumishi wangu wa kiume na kike,nitawamiminia Roho wangu siku zile,nao watatoa unabii.

19. Nitatenda miujiza juu angani,na ishara chini duniani;kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;

20. jua litatiwa giza,na mwezi utakuwa mwekundu kama damu,kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.

21. Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.’

22. “Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.

23. Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.

24. Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.

25. Maana Daudi alisema juu yake hivi:‘Nilimwona Bwana mbele yangu daima;yuko nami upande wangu wa kulia hata sitatikisika.

26. Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi;tena nilipiga vigelegele vya furaha.Mwili wangu utakaa katika tumaini,

27. maana hutaiacha roho yangu kuzimu,wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.

28. Umenionesha njia za uhai,umenijaza furaha kwa kuwako kwako!’

29. “Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.

30. Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.

Kusoma sura kamili Matendo 2