Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 15:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Basi, kanisa liliwaaga, nao walipokuwa wanapitia Foinike na Samaria waliwaeleza watu jinsi mataifa mengine yalivyomgeukia Mungu. Habari hizo zikawafurahisha sana ndugu hao wote.

4. Walipofika Yerusalemu walikaribishwa na kanisa, mitume na wazee; nao wakawapa taarifa juu ya yote Mungu aliyoyafanya pamoja nao.

5. Lakini waumini wengine waliokuwa wa kikundi cha Mafarisayo walisimama, wakasema, “Ni lazima watu wa mataifa mengine watahiriwe na kufundishwa kuifuata sheria.”

6. Basi, mitume na wazee walifanya mkutano maalumu wa kuchunguza jambo hilo.

Kusoma sura kamili Matendo 15