Agano la Kale

Agano Jipya

Marko 15:22-29 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Kisha wakampeleka Yesu mpaka mahali palipoitwa Golgotha, maana yake, mahali pa Fuvu la Kichwa.

23. Wakampa divai iliyochanganywa na manemane, lakini yeye alikataa kunywa.

24. Basi, wakamsulubisha, wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura waamue nani angepata nini.

25. Ilikuwa saa tatu asubuhi walipomsulubisha.

26. Na shtaka dhidi yake lilikuwa limeandikwa, “Mfalme wa Wayahudi.”

27. Pamoja naye waliwasulubisha wanyanganyi wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto. [

28. Hapo yakatimia Maandiko Matakatifu yanayosema, “Aliwekwa kundi moja na waovu.”]

29. Watu waliokuwa wanapita mahali hapo walimtukana, wakitikisa vichwa vyao na kusema, “Aha! Wewe mwenye kuvunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu!

Kusoma sura kamili Marko 15