Agano la Kale

Agano Jipya

1 Yohane 2:13-17 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Nawaandikieni nyinyi kina baba kwani mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo.Nawaandikieni nyinyi vijana kwa sababu mmemshinda yule Mwovu.

14. Nawaandikieni nyinyi watoto kwa sababu mnamjua Baba.Nawaandikieni nyinyi kina baba kwa kuwa mnamjua yeye ambaye amekuwako tangu mwanzo.Nawaandikieni nyinyi vijana kwa sababu mna nguvu;neno la Mungu limo ndani yenuna mumemshinda yule Mwovu.

15. Msiupende ulimwengu, wala chochote kilicho cha ulimwengu. Mtu anayeupenda ulimwengu, upendo wa Baba hauwezi kuwamo ndani yake.

16. Vitu vyote vya ulimwengu – tamaa mbaya za mwili, vitu wanavyoviona watu na kuvitamani, majivuno yasababishwayo na mali – vyote hivyo havitoki kwa Baba, bali vyatoka kwa ulimwengu.

17. Ulimwengu pamoja na vitu vyake vyote vyenye kutamanika unapita; lakini mtu atendaye atakalo Mungu, anaishi milele.

Kusoma sura kamili 1 Yohane 2