Agano la Kale

Agano Jipya

Kum. 8:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini.

5. Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo BWANA, Mungu wako, akurudivyo.

6. Nawe uzishike amri za BWANA, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

7. Kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima;

8. nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali;

Kusoma sura kamili Kum. 8