Agano la Kale

Agano Jipya

Kum. 8:2-6 Swahili Union Version (SUV)

2. Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo.

3. Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA.

4. Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arobaini.

5. Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo BWANA, Mungu wako, akurudivyo.

6. Nawe uzishike amri za BWANA, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

Kusoma sura kamili Kum. 8