Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:7-10 Swahili Union Version (SUV)

7. Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

8. Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

9. Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

10. Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.

Kusoma sura kamili Yn. 4