Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:43-49 Swahili Union Version (SUV)

43. Na baada ya siku mbili hizo akaondoka huko, akaenda Galilaya.

44. Kwa maana Yesu mwenyewe alishuhudia ya kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.

45. Basi alipotoka Galilaya, Wagalilaya walimpokea; kwa kuwa wameyaona mambo yote aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu; maana hao nao waliiendea sikukuu.

46. Basi alifika tena Kana ya Galilaya, hapo alipoyafanya yale maji kuwa divai. Na palikuwa na diwani mmoja ambaye mwanawe hawezi huko Kapernaumu.

47. Huyo aliposikia ya kwamba Yesu amekuja kutoka Uyahudi mpaka Galilaya, alimwendea, akamsihi ashuke na kumponya mwanawe; kwa maana alikuwa kufani.

48. Basi Yesu akamwambia, Msipoona ishara na maajabu hamtaamini kabisa?

49. Yule diwani akamwambia, Bwana, ushuke asijakufa mtoto wangu.

Kusoma sura kamili Yn. 4