Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 4:1-10 Swahili Union Version (SUV)

1. Kwa hiyo Bwana, alipofahamu ya kuwa Mafarisayo wamesikia ya kwamba, Yesu anafanya wanafunzi wengi kuliko Yohana, na kuwabatiza,

2. (lakini Yesu mwenyewe hakubatiza, bali wanafunzi wake,)

3. aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.

4. Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.

5. Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.

6. Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

7. Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

8. Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

9. Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

10. Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.

Kusoma sura kamili Yn. 4