Agano la Kale

Agano Jipya

Yn. 20:6-12 Swahili Union Version (SUV)

6. Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,

7. na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.

8. Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.

9. Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.

10. Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.

11. Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.

12. Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.

Kusoma sura kamili Yn. 20