Agano la Kale

Agano Jipya

Ufu. 3:5-8 Swahili Union Version (SUV)

5. Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake.

6. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.

7. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika;Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye.

8. Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu.

Kusoma sura kamili Ufu. 3