Agano la Kale

Agano Jipya

Ufu. 15:5-8 Swahili Union Version (SUV)

5. Na baada ya hayo nikaona, na hekalu la hema ya ushuhuda mbinguni lilifunguliwa;

6. na wale malaika saba, wenye mapigo saba, wakatoka katika hekalu, wamevikwa mavazi ya kitani safi, ya kung’aa, wamefungwa vifuani mwao mishipi ya dhahabu.

7. Na mmoja wa wale wenye uhai wanne akawapa wale malaika saba vitasa saba vya dhahabu, vimejaa ghadhabu ya Mungu, aliye hai hata milele na milele.

8. Hekalu likajazwa moshi uliotoka kwenye utukufu wa Mungu na uweza wake. Wala hapakuwa na mtu aliyeweza kuingia ndani ya hekalu, hata yatimizwe mapigo saba ya wale malaika saba.

Kusoma sura kamili Ufu. 15