1. Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;usiniadhibu kwa ghadhabu yako.
2. Unihurumie, ee Mwenyezi-Mungu, nimeishiwa nguvu;uniponye, ee Mwenyezi-Mungu, nataabika mpaka mifupani.
3. Ninahangaika sana rohoni mwangu.Ee Mwenyezi-Mungu, utakawia mpaka lini?
4. Unigeukie, ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe;unisalimishe kwa sababu ya fadhili zako.