Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 5:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Usikilize maneno yangu, ee Mwenyezi-Mungu,usikie ninavyopiga kite.

2. Usikilize kilio changu,Mfalme wangu na Mungu wangu,maana wewe ndiwe nikuombaye.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, alfajiri waisikia sauti yangu,asubuhi nakutolea tambiko yangu,kisha nangojea unijibu.

4. Wewe si Mungu apendaye ubaya;kwako uovu hauwezi kuwako.

Kusoma sura kamili Zaburi 5