8. Mwenyezi-Mungu atanijalia fadhili zake mchana;nami nimwimbie wimbo wa sifa usiku,nimwombe Mungu anipaye uhai.
9. Namwambia Mungu, mwamba wangu:“Kwa nini umenisahau?Yanini niende huko na huko nikiombolezakwa kudhulumiwa na adui yangu?”
10. Nimepondwa kwa matukano yao,wanaponiuliza kila siku:“Yuko wapi, Mungu wako!”
11. Mbona nasononeka hivyo moyoni?Kwa nini nahangaika hivyo?Nitamtumainia Mungu,maana nitamsifu tena Mungu,aliye msaada wangu na Mungu wangu.