Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 42:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kama paa atamanivyo maji ya kijito,ndivyo ninavyokutamani, ee Mungu wangu!

2. Naona kiu ya Mungu, kiu ya Mungu aliye hai.Nitafika lini kwake na kuuona uso wake?

3. Machozi yamekuwa chakula changu mchana na usiku,waliponiambia kila siku: “Yuko wapi Mungu Wako!”

4. Nakumbuka tena mambo hayakwa majonzi moyoni mwangu:Jinsi nilivyokwenda na umati wa watu,nikawaongoza kwenda nyumbani kwa Munguwakipiga vigelegele vya shukrani;umati wa watu wakifanya sherehe!

5. Mbona nasononeka hivyo moyoni?Kwa nini nahangaika hivyo ndani mwangu?Nitamtumainia Mungu,maana nitamsifu tenayeye aliye msaada wangu na Mungu wangu.

6. Nimesongwa na huzuni moyoni mwangu,kwa hiyo ninakukumbuka wewe, ee Mungu,kutoka katika eneo la Yordani,kutoka mlima Hermoni na Mizari.

7. Nimeporomoshewa mafuriko ya majimafuriko ya maji yaja karibunayo yaita maporomoko mapya.Mawimbi na mapigo yako yamenikumba.

Kusoma sura kamili Zaburi 42