7. Wote wanichukiao hunongonezana juu yangu;wananiwazia mabaya ya kunidhuru.
8. Husema: “Maradhi haya yatamuua;hatatoka tena kitandani mwake!”
9. Hata rafiki yangu wa moyoni niliyemwamini,rafiki ambaye alishiriki chakula changu,amegeuka kunishambulia!
10. Ee Mwenyezi-Mungu, unionee huruma!Unipe nafuu, nami nitawalipiza.
11. Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami,maadui zangu wasipopata fahari juu yangu.
12. Wewe umenitegemeza kwani natenda mema;waniweka mbele yako milele.
13. Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,tangu milele na hata milele!Amina! Amina!