1. Heri mtu anayewajali maskini;Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.
2. Mwenyezi-Mungu atamlinda na kumweka hai,naye atafanikiwa katika nchi;Mungu hatamwacha makuchani mwa maadui zake.
3. Mwenyezi-Mungu atamsaidia awapo mgonjwa,atamponya maradhi yake yote.