Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 41:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Heri mtu anayewajali maskini;Mwenyezi-Mungu atamwokoa wakati wa shida.

2. Mwenyezi-Mungu atamlinda na kumweka hai,naye atafanikiwa katika nchi;Mungu hatamwacha makuchani mwa maadui zake.

3. Mwenyezi-Mungu atamsaidia awapo mgonjwa,atamponya maradhi yake yote.

4. Nami nilisema: “Unifadhili, ee Mwenyezi-Mungu,unihurumie maana nimekukosea wewe.”

5. Madui zangu husema vibaya juu yangu:“Atakufa lini na jina lake litoweke!”

6. Wanitembeleapo husema maneno matupu;wanakusanya mabaya juu yangu,na wafikapo nje huwatangazia wengine.

7. Wote wanichukiao hunongonezana juu yangu;wananiwazia mabaya ya kunidhuru.

8. Husema: “Maradhi haya yatamuua;hatatoka tena kitandani mwake!”

9. Hata rafiki yangu wa moyoni niliyemwamini,rafiki ambaye alishiriki chakula changu,amegeuka kunishambulia!

10. Ee Mwenyezi-Mungu, unionee huruma!Unipe nafuu, nami nitawalipiza.

11. Hivyo nitajua kwamba unapendezwa nami,maadui zangu wasipopata fahari juu yangu.

12. Wewe umenitegemeza kwani natenda mema;waniweka mbele yako milele.

Kusoma sura kamili Zaburi 41