8. kutimiza matakwa yako, ee Mungu wangu ni furaha yangu,sheria yako naishika kwa moyo wangu wote!”
9. Nimesimulia habari njema za ukombozi,mbele ya kusanyiko kubwa la watu.Kama ujuavyo ee Mwenyezi-Mungu,mimi sikujizuia kuitangaza.
10. Sikuuficha moyoni mwangu ukombozi ulionijalia,nimetangaza daima kuwa wewe ni mwokozi mwaminifu;sikulificha kusanyiko kubwa la watufadhili zako na uaminifu wako.
11. Ee Mwenyezi-Mungu, usininyime huruma yako!Fadhili zako na uaminifu wako vinihifadhi daima.
12. Maafa yasiyohesabika yanizunguka,maovu yangu yanikaba hata siwezi kuona;ni mengi kuliko nywele kichwani mwangu,nami nimevunjika moyo.
13. Upende ee Mwenyezi-Mungu kuniokoa;ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.
14. Wanaonuia kuniangamiza,na waaibike na kufedheheka!Hao wanaotamani niumie,na warudi nyuma na kuaibika!
15. Hao wanaonisimanga,na wapumbazike kwa kushindwa kwao!