3. Alinifundisha wimbo mpya,wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.
4. Heri mtu anayemtumainia Mwenyezi-Mungu;mtu asiyejiunga na watu wenye majivuno,watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.
5. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, umetufanyia mengi ya ajabu,na mipango yako juu yetu haihesabiki;hakuna yeyote aliye kama wewe.Kama ningeweza kusimulia hayo yote,idadi yake ingenishinda.
6. Wewe hutaki tambiko wala sadaka,tambiko za kuteketeza wala za kuondoa dhambi;lakini umenipa masikio nikusikie.
7. Ndipo niliposema: “Niko tayari;ninayotakiwa kufanya yameandikwa katika kitabu cha sheria;
8. kutimiza matakwa yako, ee Mungu wangu ni furaha yangu,sheria yako naishika kwa moyo wangu wote!”
9. Nimesimulia habari njema za ukombozi,mbele ya kusanyiko kubwa la watu.Kama ujuavyo ee Mwenyezi-Mungu,mimi sikujizuia kuitangaza.
10. Sikuuficha moyoni mwangu ukombozi ulionijalia,nimetangaza daima kuwa wewe ni mwokozi mwaminifu;sikulificha kusanyiko kubwa la watufadhili zako na uaminifu wako.