Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 40:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nilimngojea Mwenyezi-Mungu kwa uvumilivu,akanielekea na kukisikia kilio changu.

2. Aliniondoa katika shimo la hatari,alinitoa katika matope ya dimbwi,akanisimamisha salama juu ya mwamba,na kuziimarisha hatua zangu.

3. Alinifundisha wimbo mpya,wimbo wa sifa kwa Mungu wetu.Wengi wataona na kuogopa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

4. Heri mtu anayemtumainia Mwenyezi-Mungu;mtu asiyejiunga na watu wenye majivuno,watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.

Kusoma sura kamili Zaburi 40