Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 4:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Toeni tambiko zilizo sawa,na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

6. Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”

7. Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.

8. Nalala na kupata usingizi kwa amani;ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.

Kusoma sura kamili Zaburi 4