1. Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;unionee huruma na kusikia sala yangu.
2. Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?
3. Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.
4. Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.