6. Kweli, kila mtu anapita kama kivuli;jitihada zake zote ni bure tu;anakusanya mali, asijue atakayeipata!
7. Na sasa, ee Bwana, ninatazamia nini?Tumaini langu ni kwako wewe!
8. Uniokoe katika makosa yangu yote;usikubali wapumbavu wanidhihaki.
9. Niko kama bubu, sisemi kitu,kwani wewe ndiwe uliyetenda hayo.
10. Usiniadhibu tena;namalizika kwa mapigo yako.
11. Unapomwadhibu mtu dhambi zake kwa kumkemea,unaharibu kama nondo kile akipendacho.Hakika, kila binadamu ni kama pumzi tu!
12. Usikie sala yangu, ee Mwenyezi-Mungu;usikilize kilio changu,usikae kimya ninapolia.Maana, mimi ni kama mgeni tu apitaye,ni msafiri kama walivyokuwa wazee wangu wote.