Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 39:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Kumbe umenipimia maisha mafupi sana!Maisha yangu si kitu mbele yako.Hakika, kila binadamu ni kama pumzi tu!

6. Kweli, kila mtu anapita kama kivuli;jitihada zake zote ni bure tu;anakusanya mali, asijue atakayeipata!

7. Na sasa, ee Bwana, ninatazamia nini?Tumaini langu ni kwako wewe!

8. Uniokoe katika makosa yangu yote;usikubali wapumbavu wanidhihaki.

9. Niko kama bubu, sisemi kitu,kwani wewe ndiwe uliyetenda hayo.

Kusoma sura kamili Zaburi 39