Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 39:11-13 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Unapomwadhibu mtu dhambi zake kwa kumkemea,unaharibu kama nondo kile akipendacho.Hakika, kila binadamu ni kama pumzi tu!

12. Usikie sala yangu, ee Mwenyezi-Mungu;usikilize kilio changu,usikae kimya ninapolia.Maana, mimi ni kama mgeni tu apitaye,ni msafiri kama walivyokuwa wazee wangu wote.

13. Uache kunitazama nipate kufurahi kidogo,kabla sijaaga dunia, na kutoweka kabisa.

Kusoma sura kamili Zaburi 39