Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 39:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nilisema: “Nitayachunga maisha yangu,nisije nikatenda dhambi kwa usemi wangu.Nitafunga mdomo wangu waovu wawapo karibu nami.”

2. Nilikuwa kama bubu, bila kusema kitu,nilinyamaza lakini sikupata nafuu.Mateso yangu yalizidi kuwa makali,

3. mahangaiko yangu yakaniunguza moyoni.Kadiri nilivyowaza ndivyo nilivyotaabika,kisha maneno haya yakanitoka:

4. “Ee Mwenyezi-Mungu, unijulishe mwisho wangu,siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi,nijue yapitavyo kasi maisha yangu!”

5. Kumbe umenipimia maisha mafupi sana!Maisha yangu si kitu mbele yako.Hakika, kila binadamu ni kama pumzi tu!

6. Kweli, kila mtu anapita kama kivuli;jitihada zake zote ni bure tu;anakusanya mali, asijue atakayeipata!

7. Na sasa, ee Bwana, ninatazamia nini?Tumaini langu ni kwako wewe!

8. Uniokoe katika makosa yangu yote;usikubali wapumbavu wanidhihaki.

Kusoma sura kamili Zaburi 39