Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 38:7-22 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa;mwilini mwangu hamna nafuu yoyote.

8. Nimelegea na kupondekapondeka;nasononeka kwa kusongwa moyoni.

9. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.

10. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.

11. Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.

12. Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.

13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.

14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.

15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.

16. Nakuomba tu maadui wasinisimange,wasione fahari juu ya kuanguka kwangu.

17. Karibu sana nitaanguka;nakabiliwa na maumivu ya daima.

18. Naungama uovu wangu;dhambi zangu zanisikitisha.

19. Maadui zangu hawajambo, wana nguvu;ni wengi mno hao wanaonichukia bure.

20. Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu,wananipinga kwa sababu natenda mema.

21. Usinitupe, ee Mwenyezi-Mungu;ee Mungu wangu, usikae mbali nami.

22. Uje haraka kunisaidia;ewe Mwenyezi-Mungu, uliye wokovu wangu.

Kusoma sura kamili Zaburi 38