7. Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa;mwilini mwangu hamna nafuu yoyote.
8. Nimelegea na kupondekapondeka;nasononeka kwa kusongwa moyoni.
9. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.
10. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.
11. Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.
12. Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.
13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.
14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.
15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.
16. Nakuomba tu maadui wasinisimange,wasione fahari juu ya kuanguka kwangu.
17. Karibu sana nitaanguka;nakabiliwa na maumivu ya daima.
18. Naungama uovu wangu;dhambi zangu zanisikitisha.
19. Maadui zangu hawajambo, wana nguvu;ni wengi mno hao wanaonichukia bure.
20. Hao wanaonilipa maovu kwa wema wangu,wananipinga kwa sababu natenda mema.
21. Usinitupe, ee Mwenyezi-Mungu;ee Mungu wangu, usikae mbali nami.
22. Uje haraka kunisaidia;ewe Mwenyezi-Mungu, uliye wokovu wangu.