Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 38:5-15 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Madonda yangu yameoza na kunuka,na hayo ni matokeo ya ujinga wangu.

6. Nimepindika mpaka chini na kupondeka;mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.

7. Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa;mwilini mwangu hamna nafuu yoyote.

8. Nimelegea na kupondekapondeka;nasononeka kwa kusongwa moyoni.

9. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.

10. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.

11. Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.

12. Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.

13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.

14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.

15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.

Kusoma sura kamili Zaburi 38