5. Madonda yangu yameoza na kunuka,na hayo ni matokeo ya ujinga wangu.
6. Nimepindika mpaka chini na kupondeka;mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
7. Viungo vyangu vimeshambuliwa na homa;mwilini mwangu hamna nafuu yoyote.
8. Nimelegea na kupondekapondeka;nasononeka kwa kusongwa moyoni.
9. Ee Bwana, wewe wajua tazamio langu lote;kwako hakikufichika kilio changu.
10. Moyo wanidunda, nguvu zimeniishia;hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.
11. Rafiki na wenzangu wanaepa kuona mateso yangu,na jamaa zangu wanakaa mbali nami.
12. Wanaotaka kuniua wanatega mitego yao;wanaonitakia niumie wanatishia kuniangamiza.Mchana kutwa wanafanya mipango dhidi yangu.
13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.
14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.
15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.