Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 38:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;usiniadhibu kwa ghadhabu yako.

2. Mishale yako imenichoma;mkono wako umenigandamiza.

3. Hamna mahali nafuu mwilini mwangu,kwa sababu umenikasirikia;hamna penye afya hata mifupani mwangu,kwa sababu ya dhambi yangu.

4. Nimefunikwa kabisa na dhambi zangu,zinanilemea kama mzigo mzito mno kwangu.

5. Madonda yangu yameoza na kunuka,na hayo ni matokeo ya ujinga wangu.

Kusoma sura kamili Zaburi 38