6. Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama
7. Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.
8. Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;wawanywesha kutoka mto wa wema wako.
9. Wewe ndiwe asili ya uhai;kwa mwanga wako twaona mwanga.
10. Uendelee kuwafadhili wale wanaokutambua;uzidi kuwa mwema kwa wanyofu wa moyo.
11. Usikubali wenye majivuno wanivamie,wala watu waovu wanikimbize.