3. Kila asemacho ni uovu na uongo;ameacha kutumia hekima na kutenda mema.
4. Alalapo huwaza kutenda maovu,hujiweka katika njia isiyo njema,wala haachani na uovu.
5. Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;uaminifu wako wafika mawinguni.
6. Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama
7. Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.
8. Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;wawanywesha kutoka mto wa wema wako.
9. Wewe ndiwe asili ya uhai;kwa mwanga wako twaona mwanga.