Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 36:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Dhambi huongea na mtu mwovu,ndani kabisa moyoni mwake;jambo la kumcha Mungu halimo kabisa kwake.

2. Mwovu hujipendelea mwenyewe,hufikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.

3. Kila asemacho ni uovu na uongo;ameacha kutumia hekima na kutenda mema.

4. Alalapo huwaza kutenda maovu,hujiweka katika njia isiyo njema,wala haachani na uovu.

5. Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;uaminifu wako wafika mawinguni.

6. Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama

Kusoma sura kamili Zaburi 36