9. Mcheni Mwenyezi-Mungu enyi watakatifu wake;maana wenye kumcha hawatindikiwi na kitu.
10. Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.
11. Njoni enyi vijana mkanisikilize,nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.
12. Je, watamani kufurahia maisha,kuishi maisha marefu na kufurahia mema?
13. Basi, acha kusema mabaya,na kuepa kusema uongo.
14. Jiepushe na uovu, utende mema;utafute amani na kuizingatia.
15. Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,na kusikiliza malalamiko yao;
16. lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.
17. Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.
18. Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.