7. Malaika wa Mwenyezi-Mungu huwalinda wote wamchao,na kuwaokoa katika hatari.
8. Jaribuni mwone Mwenyezi-Mungu alivyo mwema.Heri mtu anayekimbilia usalama kwake.
9. Mcheni Mwenyezi-Mungu enyi watakatifu wake;maana wenye kumcha hawatindikiwi na kitu.
10. Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.
11. Njoni enyi vijana mkanisikilize,nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.
12. Je, watamani kufurahia maisha,kuishi maisha marefu na kufurahia mema?
13. Basi, acha kusema mabaya,na kuepa kusema uongo.
14. Jiepushe na uovu, utende mema;utafute amani na kuizingatia.
15. Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,na kusikiliza malalamiko yao;
16. lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.
17. Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.
18. Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
19. Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.
20. Huvilinda viungo vya mwili wake wote,hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.
21. Ubaya huwaletea waovu kifo;wanaowachukia waadilifu wataadhibiwa.
22. Mwenyezi-Mungu huokoa maisha ya watumishi wake,wote wanaomkimbilia hawataadhibiwa.