Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 34:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi-Mungu,wanyonge wasikie na kufurahi.

3. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu pamoja nami,sote pamoja tulisifu jina lake.

4. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu,na kuniondoa katika hofu zangu zote.

5. Mgeukieni Mungu mpate kufurahi;nanyi hamtaaibishwa kamwe.

6. Maskini alimlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamsikia,na kumwokoa katika taabu zake zote.

Kusoma sura kamili Zaburi 34