Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 34:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.

17. Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.

18. Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.

19. Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.

20. Huvilinda viungo vya mwili wake wote,hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.

21. Ubaya huwaletea waovu kifo;wanaowachukia waadilifu wataadhibiwa.

22. Mwenyezi-Mungu huokoa maisha ya watumishi wake,wote wanaomkimbilia hawataadhibiwa.

Kusoma sura kamili Zaburi 34