1. Nitamtukuza Mwenyezi-Mungu nyakati zote,sitaacha kamwe kuzitamka sifa zake.
2. Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi-Mungu,wanyonge wasikie na kufurahi.
3. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu pamoja nami,sote pamoja tulisifu jina lake.
4. Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu,na kuniondoa katika hofu zangu zote.
5. Mgeukieni Mungu mpate kufurahi;nanyi hamtaaibishwa kamwe.
6. Maskini alimlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamsikia,na kumwokoa katika taabu zake zote.
7. Malaika wa Mwenyezi-Mungu huwalinda wote wamchao,na kuwaokoa katika hatari.
8. Jaribuni mwone Mwenyezi-Mungu alivyo mwema.Heri mtu anayekimbilia usalama kwake.
9. Mcheni Mwenyezi-Mungu enyi watakatifu wake;maana wenye kumcha hawatindikiwi na kitu.
10. Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.
11. Njoni enyi vijana mkanisikilize,nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.
12. Je, watamani kufurahia maisha,kuishi maisha marefu na kufurahia mema?
13. Basi, acha kusema mabaya,na kuepa kusema uongo.
14. Jiepushe na uovu, utende mema;utafute amani na kuizingatia.
15. Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,na kusikiliza malalamiko yao;
16. lakini huwapinga watu watendao maovu,awafutilie mbali kutoka duniani.
17. Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,na kuwaokoa katika taabu zao zote.
18. Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
19. Mateso ya mwadilifu ni mengi,lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.