Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 33:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Dunia yote na imwogope Mwenyezi-Mungu!Wakazi wote duniani, wamche!

9. Maana alisema na ulimwengu ukawako;alitoa amri nao ukajitokeza.

10. Mwenyezi-Mungu hupangua mipango ya mataifa,na kuyatangua mawazo yao.

11. Mpango wa Mwenyezi-Mungu hudumu milele;maazimio yake yadumu vizazi vyote.

12. Heri taifa ambalo Mungu wake ni Mwenyezi-Mungu;heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe!

13. Mwenyezi-Mungu huangalia chini kutoka mbinguni,na kuwaona wanadamu wote.

Kusoma sura kamili Zaburi 33