Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 33:5-11 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mungu apenda uadilifu na haki,dunia imejaa fadhili za Mwenyezi-Mungu.

6. Mbingu ziliumbwa kwa neno la Mwenyezi-Mungu,na vyote vilivyomo kwa pumzi ya mdomo wake.

7. Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa,vilindi vya bahari akavifunga ghalani.

8. Dunia yote na imwogope Mwenyezi-Mungu!Wakazi wote duniani, wamche!

9. Maana alisema na ulimwengu ukawako;alitoa amri nao ukajitokeza.

10. Mwenyezi-Mungu hupangua mipango ya mataifa,na kuyatangua mawazo yao.

11. Mpango wa Mwenyezi-Mungu hudumu milele;maazimio yake yadumu vizazi vyote.

Kusoma sura kamili Zaburi 33