Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 33:15-22 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Yeye huunda mioyo ya watu wote,yeye ajua kila kitu wanachofanya.

16. Mfalme hawezi kuokolewa kwa kuwa na jeshi kubwa;wala shujaa hapati ushindi kwa nguvu zake kubwa.

17. Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi;nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mtu.

18. Mwenyezi-Mungu huwaangalia wale wamchao,watu ambao wanatumainia fadhili zake.

19. Yeye huwaokoa katika kifo,huwaweka hai wakati wa njaa.

20. Mioyo yetu yamtumainia Mwenyezi-Mungu.Yeye ni msaada wetu na ngao yetu.

21. Naam twafurahi kwa sababu yake;tuna matumaini katika jina lake takatifu.

22. Fadhili zako zikae nasi, ee Mwenyezi-Mungu,kwani sisi tumekuwekea tumaini letu.

Kusoma sura kamili Zaburi 33