Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 33:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu!Kumsifu Mungu ni wajibu wa watu wanyofu.

2. Msifuni Mwenyezi-Mungu kwa zeze;mwimbieni kwa kinubi cha nyuzi kumi.

3. Mwimbieni wimbo mpya;pigeni kinubi vizuri na kushangilia.

4. Neno la Mwenyezi-Mungu ni la kweli;na matendo yake yote ni ya kuaminika.

5. Mungu apenda uadilifu na haki,dunia imejaa fadhili za Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili Zaburi 33