1. Shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu!Kumsifu Mungu ni wajibu wa watu wanyofu.
2. Msifuni Mwenyezi-Mungu kwa zeze;mwimbieni kwa kinubi cha nyuzi kumi.
3. Mwimbieni wimbo mpya;pigeni kinubi vizuri na kushangilia.
4. Neno la Mwenyezi-Mungu ni la kweli;na matendo yake yote ni ya kuaminika.
5. Mungu apenda uadilifu na haki,dunia imejaa fadhili za Mwenyezi-Mungu.