4. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa, enyi waaminifu wake;kumbukeni utakatifu wake na kumshukuru.
5. Hasira yake hudumu kitambo kidogo,wema wake hudumu milele.Kilio chaweza kuwapo hata usiku,lakini asubuhi huja furaha.
6. Mimi nilipofanikiwa, nilisema:“Kamwe sitashindwa!”
7. Kwa wema wako, ee Mwenyezi-Mungu,umeniimarisha kama mlima mkubwa.Lakini ukajificha mbali nami,nami nikafadhaika.