Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 30:1-11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, nakutukuza maana umeniokoa,wala hukuwaacha maadui zangu wanisimange.

2. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu,nilikulilia msaada, nawe ukaniponya.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, umeniokoa kutoka kuzimu;umenipa tena uhai,umenitoa miongoni mwa waendao kuzimu.

4. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa, enyi waaminifu wake;kumbukeni utakatifu wake na kumshukuru.

5. Hasira yake hudumu kitambo kidogo,wema wake hudumu milele.Kilio chaweza kuwapo hata usiku,lakini asubuhi huja furaha.

6. Mimi nilipofanikiwa, nilisema:“Kamwe sitashindwa!”

7. Kwa wema wako, ee Mwenyezi-Mungu,umeniimarisha kama mlima mkubwa.Lakini ukajificha mbali nami,nami nikafadhaika.

8. Nilikulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;naam niliomba dua kwako ee Mwenyezi-Mungu:

9. “Je, utapata faida gani nikifana kushuka hadi kwa wafu?Je, mavumbi ya wafu yanaweza kukusifu?Je, yanaweza kusimulia uaminifu wako?

10. Usikie, ee Mwenyezi-Mungu, unihurumie;ee Mwenyezi-Mungu, unisaidie!”

11. Wewe umegeuza maombolezo langu kuwa ngoma ya furaha;umeniondolea huzuni yangu, ukanizungushia furaha.

Kusoma sura kamili Zaburi 30