Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 29:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Huirusha milima ya Lebanoni kama ndama,milima ya Sirioni kama mwananyati.

7. Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutoa miali ya moto.

8. Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa,Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa la Kadeshi.

9. Sauti ya Mwenyezi-Mungu huitikisa mivule,hukwanyua majani ya miti msituni,na hekaluni mwake wote wasema:“Utukufu kwa Mungu!”

10. Mwenyezi-Mungu ameketi juu ya gharika;Mwenyezi-Mungu ni mfalme atawalaye milele.

11. Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!

Kusoma sura kamili Zaburi 29