6. Huirusha milima ya Lebanoni kama ndama,milima ya Sirioni kama mwananyati.
7. Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutoa miali ya moto.
8. Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa,Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9. Sauti ya Mwenyezi-Mungu huitikisa mivule,hukwanyua majani ya miti msituni,na hekaluni mwake wote wasema:“Utukufu kwa Mungu!”
10. Mwenyezi-Mungu ameketi juu ya gharika;Mwenyezi-Mungu ni mfalme atawalaye milele.
11. Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!