Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 27:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Hata kama wazazi wangu wakinitupa,Mwenyezi-Mungu atanipokea kwake.

11. Unifundishe njia yako, ee Mwenyezi-Mungu;uniongoze katika njia iliyo sawa,kwa sababu ya maadui zangu.

12. Usiniache maadui wanitende wapendavyo;maana mashahidi wa uongo wananikabili,nao wanatoa vitisho vya ukatili.

13. Naamini nitauona wema wake Mwenyezi-Mungukatika makao ya walio hai.

14. Mtegemee Mwenyezi-Mungu!Uwe na moyo, usikate tamaa!Naam, mtegemee Mwenyezi-Mungu!

Kusoma sura kamili Zaburi 27