9. Huwaongoza wanyenyekevu katika uadilifu;naam, huwafundisha hao njia yake.
10. Mwenyezi-Mungu hutenda kwa fadhili na uaminifu,kwa wale wanaoshika agano lake na maamuzi yake.
11. Kwa ajili ya jina lako, ee Mwenyezi-Mungu,unisamehe kosa langu kwani ni kubwa.
12. Kila mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,Mwenyezi-Mungu atamfunza njia ya kufuata.
13. Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima,na wazawa wake watamiliki nchi.
14. Mwenyezi-Mungu ni rafiki ya wale wamchao;yeye huwajulisha hao agano lake.
15. Namwangalia Mwenyezi-Mungu daima;yeye atainasua miguu yangu mtegoni.
16. Unielekee, ee Mungu, unionee huruma,maana mimi ni mpweke na mnyonge.
17. Uniondolee mahangaiko ya moyoni mwangu;unitoe katika mashaka yangu.
18. Uangalie mateso yangu na dhiki yangu;unisamehe dhambi zangu zote.
19. Angalia jinsi walivyo wengi maadui zangu;ona jinsi wanavyonichukia kwa ukatili.
20. Uyalinde maisha yangu, uniokoe;nakimbilia usalama kwako,usikubali niaibike.
21. Wema na uadilifu vinihifadhi,maana ninakutumainia wewe.
22. Ee Mungu, uwaokoe watu wako, Israeli;uwaokoe katika taabu zao zote.