Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 25:9-15 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Huwaongoza wanyenyekevu katika uadilifu;naam, huwafundisha hao njia yake.

10. Mwenyezi-Mungu hutenda kwa fadhili na uaminifu,kwa wale wanaoshika agano lake na maamuzi yake.

11. Kwa ajili ya jina lako, ee Mwenyezi-Mungu,unisamehe kosa langu kwani ni kubwa.

12. Kila mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,Mwenyezi-Mungu atamfunza njia ya kufuata.

13. Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima,na wazawa wake watamiliki nchi.

14. Mwenyezi-Mungu ni rafiki ya wale wamchao;yeye huwajulisha hao agano lake.

15. Namwangalia Mwenyezi-Mungu daima;yeye atainasua miguu yangu mtegoni.

Kusoma sura kamili Zaburi 25